Phesto

TUKIYASOMA MAANDIKO

May 21, 2025

TUKIYASOMA MAANDIKO

1.S: Tukiyasoma maandiko ooh ya kale yale yaliyotabiriwa na manabii
Nabii Isaya alitabiri na Yohana mbatizaji naye hivyo hivyo, atazaliwa Masiya katika hali ya umasikini, (Kazaliwa kwa taabu kafundisha kwa taabu Yesu kisha walimtesa na kumuua Golgata) x2

2. S: Walidhani ndio mwisho wake Bwana Yesu walipomsulubisha pale msalabani
Kina mama watatu walishangaa walipoona lile jiwe limeondolewa walisahau ya kwamba hakika Yesu yeye alisema
(ilimpasa kufa siku ya tatu kufufuka yeye simba wa Yuda na Leo hii yuko hai) x2

3. S: Yesu ni yeye yule jana Leo hata milele, ukimpokea yeye utayashinda yote
Damu yake ya thamani ilimwagika kutuosha dhambi zetu sisi wanadamu kutupatanisha Yesu na Baba Mungu wetu wa mbinguni ndugu tumpokee tufanyike wana wa Mungu ili kibali tupate na mbinguni tuingie x2

CHORUS :
Amefufuka Leo amefufuka
Yesu ameshinda mauti amefufuka
S: Haya twendeni
W: Haya twendeni jama haya twendeni tukalione kaburi lake liwazi.

Article by Phesto

Lorem ipsum amet elit morbi dolor tortor. Vivamus eget mollis nostra ullam corper. Natoque tellus semper taciti nostra primis lectus donec tortor fusce morbi risus curae. Semper pharetra montes habitant congue integer nisi.

Leave a Comment